Posts

MICHEZO KITAIFA KIMATAIFA UTAMADUNI

TULITAKA 6 TUMEPA MANNE

Image
Wachonga vitanda Wa Kwerekwe waendeleza wimbi la ushindi mashindano ya elimu bila malipo VTA. Chuo cha mwanakwerekwe VT kimepata mapumziko mazuri baada ya ushindi mnono Wa goli nne kwa mbili dhidi ya Experience Mchezo uliochezwa viwanja vya Olympic Dole majira ya saa nne na nusu asubuhi ya Leo. Mchezo huo ulioanza kwa mashambulizi kwa timu ya Chuo cha Kwerekwe nakupelekea kupata goli la mapema dakika ya kwanzaa ya mchezo huo     Mchezo uliwalazimu kuanza  kwa mchezaji Wa Chuo cha  Experience dakika 10 baadae kuoneshwa kadi nyekundu kwa kosa la kuunawa mpira mithili ya mchuzi wa chukuchiku na kuifanya icheze pungufu kwa Muda mwingi Wa Mchezo huo.   Michezo mengine iliyochezwa Leo mafundi magari wa mkokotoni wakiwafundisha kupangua gear box mafundi umeme Wa karume,kwa ushindi wa goli moja bila majibu. wafunga Bomba Wa Mombasa Al mubarak wakiteleza na ushindi wasiwoutolea jasho baada ya wajukuu Wa mama Samia Assalam kushindwa kufika uwanjani kwa wakati  H...

Mashindano ya Polisi Jamii magharibi B

MASHINDANO YA POLISI JAMII CUP WILAYA MAGHARIBI B YALIENDELEA TENA LEO KWA VIWANJA VIWILI TOFAUTI.KIWANJA CHA KIEMBE SAMAKI KISAUNI FC WALIWEKA MPIRA KWAPANI HAWAKUFIKA UWANJANI NA USHINDI WA MAGOLI MAWILI NA POINT TATU WAMECHUKUA CHUKWANI BUYU FC.  KATIKA KIWANJA CHA NGOME ILIKUWA NI MPAMBANO KATI YA NEW GENERATION FC NA MILIMANI FC MATOKEO ,NEW GENERATION FC WAMESHINDA MABAO 3 NA MILIMANI WAMEPATA BAO MOJA GOLI LA MILIMANI LILIPATIKANA KIPINDI CHA PILI DAKIKA YA 70 LILIFUNGWA NA OMAR SAID NA MAGOLI YA NEW GENERATION FC YALIFUNGWA KIPINDI CHA PILI DAKIKA YA 75  LILIFUNGWA NA ABDI HASSAN NA PILI DAKIKA YA 81 LILIFUNGWA NA NASSORO ALI   NA LA TATU LILIFUNGWA NA AHMED MAHMUD DAKIKA YA 84           AIDHA MWENYEKITI WA KAMATI YA MAANDALIZI YA MASHINDANO HAYO AMBAE NI MKUU WA KITUO CHA POLISI MAZIZINI SP- SALUM NGAYANA ALITUMIA MUDA MFUPI KUTOA ELIMU KWA WANANCHI KUIMARISHA USHIRIKIANO AND ULINZI SHIRIKISHI KATIKA SHEHIA ZAO. KESHO MASHINDANO...

MAITI YANG'ANG'ANIIA JENENZA

Image
 Mvua yawapatia suluhu Al-Asaah licha ya ugeni wao mbele ya wenyeji Wa mashindano hayo Experience VTC . Mchezo Wa kwanza Wa mashindano ya elimu bila malipo kwa mkoa wa mafunzo ya Amali umekamilika kwa kugawanya alama vyuo hivyo hapo katika viunga vya MAO the Dong asubuhi ya Leo. Katika Mchezo huo ulishuhudia mchezaji  chuo cha.Experience akiwa Wa kwanzaa kupigwa umeme akiyaanza vibaya mashindano hayo kwa ajili ya kunusuru timu yake kupata aibu mbele ya vyuo mbali mbali vilivyokuepo uwanjani hapo. Mechi Nyengine zitachezwa hapo kesho kwa michezo miwili Mubarrak Al Mazrui vs Makunduchi ,JKU vs Adult Forodhani Karume vs ICPS , Al-Asaah VTC vs Kwerekwe
Image
 Wizara ya afya Zanzibar kwa kushirikian na taasisi ya THE SAME QUALITY FOUNDATION wameendesha kambi ya matibabu ya midomo wazi katika hospitali ya mkoa Lumumba ikiwa ni muendelezo wa kambi zinazofanywa na taasisi hio ili kuhakikisha watoto wenye tatizo la midomo wazi wanapatiwa matibabu. Akizungumza katika kambi hio Mkurugenzi na muazilishi wa Taasisi hio Dr Piter Mabula amesema takriban miaka kumi na moja taasisi hio imekua ikitoa huduma hio na imefanikiwa kufanya matibabu wa watu zaid ya 2500 kwa Tanzania bara na visiwani ambapo kwa zanzibbar zaid ya watu 200 wamepatiwa huduma hio Dr Piter Mabula Mkurugenzi wa taasisi ya THE SAME QUALITY FOUNDATION Kwa upande wake Dr Sumaiya Said Abud kutoka katika hospitali ya mkoa Lumumba amesema kambi hio ya siku tano inatarajia kufanya matibabu ya watoto 25 ambao tayar watoto hao wamefanyiwa uchunguzi wa awali Dr Sumaiya Said Abud hospitali ya mkoa Lumumba Sambamba na hayo sumaiya ametoa wito kwa wazazi na walezi wenye watoto wenye...

Mshike mshike wa Polisi Jamii Cup magharibi B

Image
MASHINDANO YA POLISI JAMII CUP WILAYA MAGHARIBI B YALIENDELEA TENA KWENYE VIWANJA VIWILI TOFAUTI.KWENYE DIMBA LA  KIEMBE SAMAKI KULIKUWA NA PAMBANO KATI YA NYAMANZI CITY NA CHUNGA CITY MATOKEO IKIWA NI GOLI  4 KWA  1 MAGOLI YA CHUNGA YALIFUNGWA NA YASSIR MOHD DAKIKA YA 7 NA GOLI LA PILI  LILIFUNGWA TENA NA YASSIR MOHD DAKIKA YA 12. NA BAO LA KUFUTIA MACHOZI LA NYAMANZI CITY LIMEFUNGWA DAKIKA YA 39 NYAMANZI WALIPATA BAO LA KUFUTIA MACHOZI LILILOFUNGWA NA JUMA KOTO .DAKIKA YA 68 SAID SALUM ALIPATIA TENA CHUNGA CITY BAO LA TATU NA DAKIKA YA78 EVEREST ALIPATIA CHUNGA CITY GOLI LA NNE. KWENYE MCHEZO HUO  MWENYEKITI WA KAMATI YA MAANDALIZI YA MASHINDANO YA POLISI JAMII CUP NA MKUU WA KITUO CHA POLISI MAZIZINI SP- SALUM NGAYANA ALIMKABIDHI MPIRA YASSIR MOHD KWA KUWA MAN OF THE MATCH ALIPATIA MABAO MAWILI NA ASSIST MBILI . KULE DIMBA LA NGOME KULIKUWA NA MPAMBANO KATI YA SHUBA SHUBA FC NA KOMBENI FC MATOKEO NI KOMBENI FC WAMESHINDA KWA PENATI 5 KWA 4 DHIDI YA SHUBA SHU...

KMKM yaondoka na alama tatu kibindoni kio

Image
Akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kukamilika kwa mchezo huo kocha msaidizi wa Ibrahim Khamis Khatib amesema wapinzani wao walikuja kwa kupania mchezo ndio kilichowafanya washinde magoli wawili. Amesema mchazaji samir ametoka kwenye majeraha ndio maana hayukp vizuri. Ibrahim amewataka washabiki wa KMKM kuja viwanjani kuona kandanda inavyochezwa. Nae kocha wa muembe makumbi Rajab Mrisho amesema waamuzi bado wana mapungufu ndio maana wamepoteza mchezo wa leo. Amesema mchezo ulianza vizuri kipindi cha kwanza mabadiliko yamekuja kipindi cha pili amedai licha ya mchezo kwenda nao vizuri, wachezaji wake wamejituma wakishindwa kwenye mipango na kupelekea kufungwa goli mbili kwa moja.

Historia ya Majestic cinema.

Image
Historia Ya Majestic Cinema Na  Kuunguwa  Moto. Majestic Cinema, iliyofunguliwa mnamo Oktoba 20, 1955, baada ya jengo la kwanza la sinema kuunguwa, ilikuwa ni fahari ya Zanzibar, Ilibuniwa na mbunifu maarufu  Mzanzibari Dayalji Pitamber Sachania, baada ya sinema ya awali, Royal Cinema iliyojengwa 1921, kuteketea kwa moto mnamo Februari 8, 1954 ,siku hiyo kulikuwa na Zanana show ,ingawa nje kulikuwa na mabarobaro tele wakitia macho nuru, siku ambayo ikiendeshwa filamu inayoitwa Albela.Albela ni filamu ya vichekesho na  muziki ya Bollywood ya 1951 iliyoongozwa na nyota Bhagwan Dada na Geeta Bali. Sinema  Yakihindi ilikuwa ya  kwanza kwa  mapato ya juu kwa wakati huo na sinema ilijaa wanawake ikaleta mtafaruku mkubwa  . Royal Cinema, iliyokuwa sinema ya kwanza ya kifahari katika Afrika Mashariki, ilifunguliwa na Hassanali Adamjee Jariwalla na kubuniwa na J.H. Sinclair,  Majestic Cinema ilikuwa na muundo  mpya wa kipekee wa vishubaka vya mis...